
Mgombea udiwani wa Kata ya Makurumla ,Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Mkoani Dar es Salam, kupitia CCM Bakari Kimwanga leo Agosti 19,2025 amechukua fomu ya kuwania udiwani.
Akizungumza baada ya kuchukua fomu amesema kuwa anaamini anakwenda kutekeleza ahadi zote alizoahidi huku akiwaomba wananchi ifikapo Oktoba 29, mwaka huu kumchagua kwa kura nyingi Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, Mbunge wa CCM na diwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).









