Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dk Emmanuel Nchimbi alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Chake Chake kisiwani Pemba kwa ajili ya kwenda kufanya mkutano wa kampeni katika eneo la Kinyasi, wilayani Wete leo Oktiba 8, 2025.
Dk Nchimbi anafanya mkutano huo kwa ajili ya kumuombea kura Mgombea urais wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan, Mgombea urais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi, wagombea wa ubunge, uwakilishi pamoja na udiwani.