Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Wachezaji timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo
*
Mgodi wa Barrick Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, umeendelea kujenga uhusiano mzuri na jamii za maeneo yanaozunguka mgodi kupitia jukwaa la michezo ambapo Oktoba 14,2025 timu ya mpira wa kikapu inayoundwa na wafanyakazi wa mgodi iliikaribisha timu ya Sixers kutoka Kahama katika mechi ya kirafiki ambapo Bulyanhulu imeibuka na ushindi wa vikapu 33-30.
Migodi ya Barrick ya Bulyanhulu na North Mara inazo programu za kuwawezesha wafanyakazi wake kushiriki katika michezo mbalimbali kwa ajili ya kujenga afya zao.
Pia imekuwa ikiandaa mashindano mbalimbali yanayojumuisha jamii za maeneo yanayozunguka mgodi kwa ajili ya kujenga uhusiano mzuri na kuzipatia fursa kufahamu shughuli za migodi hiyo.
Wachezaji timu ya Sixers wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo
Wachezaji timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo
Wachezaji timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers wakipata maelekezo kabla ya mchezo
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakifuatilia mchezo