Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Februari 28, 2026 ameshiriki mazishi ya Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, yaliyofanyika katika Kanisa la Hija ya Bikira Maria – Pugu, jijini Dar es Salaam.
Mazishi hayo yameongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi na kuhudhuriwa na viongozi wengine wa Serikali pamoja na viongozi wa dini mbalimbali.




