Na. Vero Ignatus Arusha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa amewasili Mkoani Arusha na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Paul Christian Makonda pamoja na viongozi wengine wa Serikali na Chama leo tarehe 28 Aprili, 2025.
Waziri Mkuu anatarajia kufungua Mkutano wa 73 wa Baraza la Kimataifa la viwanja vya ndege kwa kanda ya Afrika (ACI Afrika) unaofanyika kwenye Hotel ya Mount Meru.
Awali akitoa salamu kwa mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda Arusha amemshukuru Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
kwa kuridhia uwanja huo mzuri wa kisasa katika mkoa wa Arusha ambapo unaweza ukawa namba moja basi ama namba mbili katika nchi ya Tanzania .
Vile vile ameshukuru Prof. Godius Walter Kahyarara Katibu Mkuu wa Wizara kwa kuridhiwa uwanja huo kutumika kwa ndege ndogo zinazounganisha Afrika ya Mashariki kwa wageni wanaotaka kutua katika uwanja huo
“Nafahamu hatua zinaendelea vizuri na siyo muda mrefu Mamlaka watatangaza ya kwamba Arusha unaweza kutumia sasa uwanja wa ndege kama point of interest na kuwaruhusu wageni wenye private jet kuja Arusha bila kuhangaika kwenda Kilimanjaro. Alisema Makonda.