Aliyekuwa mbunge wa Dodoma Mjini Antony Mavunde ameibuka mshindi katika kura za maoni za Ubunge za Chama Cha Mapinduzi CCM katika Jimbo jipya la Mtumba Mkoani Dodoma
Mavunde amepata kura 6,076 kati ya kura halali 7,330 zilizopigwa ikiwa ni sawa na asilimia ya 83 ya kura zote na kuwaacha wagombea wenzake wanne waliokuwa wakichuana naye.