Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa dini mara baada ya kuwasili Maramba mkoani Tanga kushiriki Ibada Maalum ya kumuombea aliyekuwa Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Marehemu Dkt. Stephen Munga, iliyofanyika, Maramba Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisaini kitabu cha maombolezo wakati alipowasili nyumbani kwa aliyekuwa Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Marehemu Dkt. Stephen Munga, kushiriki Ibada Maalum ya kumuombea Askofu huyo, Maramba mkoani Tanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akishiriki Ibada Maalum ya kumuombea aliyekuwa Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Marehemu Dkt. Stephen Munga, iliyofanyika, Maramba Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wakiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Marehemu Dkt. Stephen Munga wakati wa Ibada maalum ya kumuombea Askofu huyo, iliyofanyika, Maramba Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wakifanya maombi pamoja na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa pamoja na Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga Mhashamu Thomas Kiangio mara baada ya Ibada Maalum ya kumuombea aliyekuwa Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Marehemu Dkt. Stephen Munga, iliyofanyika, Maramba Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.